WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na maandalizi ya sherehe za miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayoendelea katika Uwanja wa Jamuhuri mjini Dodoma.
Ameyasema hayo leo (Jumanne, Aprili 24, 2018) mara baada ya kukagua maandalizi hayo yanayofanyika kwenye Uwanja wa Jamuhuri mjini Dodoma, ambapo amesema maandalizi yanaendelea vizuri.
Waziri Mkuu amejionea maonesho mbalimbali yakiwemo ya kikundi cha halaiki ambacho kinaundwa na wanafunzi 2,000 kutoka Manispaa ya Dodoma pamoja na maonyesho ya kujihami na maadui yaliyooneshwa na Jeshi la Magereza.
“Nimeridhika na kazi ambayo mmeifanya, nawaruhusu muendelee kushirikiana katika kukamilisha maeneo ambayo yamesalia na kuanzia kesho tujiandae kuwapokea wageni kutoka maeneo mbalimbali.”
Alhamisi Aprili 26, 2018 Watanzania wanatarajia kuadhimisha miaka 54 ya Muungano tangu Tanganyika ilipoungana na Zanzibar, chini ya waasisi wake Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama onesho lahalaiki, wakati alipokagua
maandalizi ya sherehe za miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,
kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 24, 2018. Kutoka kulia ni
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera na Uratibu) Profesa Faustine
Kamuzola, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilinith Mahenge, Waziri wa Nchi
Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu ,
Jenista Mhagama, Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga
Taifa, Dr Florens Turuka, naMkuu wa Majeshi ya Tanzania, Jenerali
Venance Mabeyo.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Askari
wa Jeshi la Magereza, wakionesha zoezi la kupambana na adui mbele
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wakati alipokagua maandalizi ya sherehe za
miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwenye uwanja wa
Jamhuri mjini Dodoma Aprili 24, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa, akiwapungia wananchi, wakati alipokagua
maandalizi ya sherehe za miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,
katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 24, 2018.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...