Na Agness Francis, Globu ya Jamii.

WIZARA ya Afya,Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto imewataka watoa huduma za kimaabara kwa wananchi kuhakikisha wanakuwa na vibali, kwani kinyume na hapo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao kwa mujibu wa sheria.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo , Mkurugenzi Msaidizi Huduma ya uchunguzi na magonjwa Dk. Charles Massambu amesisitiza sheria itachukua mkondo wake kwa wale wanaohudumia wananchi shughuli za kimaabara lakini hawana vibali au kusajiliwa.

"Hakuna mtoa huduma atakaetoa huduma za maabara bila kusajiliwa.Tukibaini tutamchukulia hatua kali za kisheria," amesema Dkt. Massambu.

Aidha Massambu ameeleza baraza linatambua uwezo na utaalamu katika kuelimisha jamii ya watanzania kuhusu majukumu katika kuwahudumia.Pia kutokana na changamoto za majibu ya vipimo kutofautiana kutoka sehemu moja hadi nyingine , Wizara imechukua hatua ya uhakiki wa ubora wa vipimo.

"Tanzania kuna maabara 33 ambazo ni nyota moja mpaka nne,nyingine nane zilizo na hadhi ya kimataifa ambapo vipimo vyake huwa ni sawa na vya nchi nyingine za nje.
 Mkurugenzi msaidizi wa huduma za uchunguzi wa Magonjwa Dkt Charles G Massambu akizungumza na waandishi wa habari leo katika ofisi zao Jijini Dar es Salaam akiwataka watoa huduma ya maabara wasio na vibali kutoka baraza la wataalamu la maabara  kujisajili au kuacha kufanya kazi hiyo.
 Msajili wa Baraza la wataalamu wa maabara akizungumza na waandishi wa habari leo katika ofisi zao Jijini Dar es Salaam akielezea kuhusu umuhimu wa kusajili huduma hizo.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...