Na Zainab Nyamka, Globu ya jamii

SHIRIKISHO la Mpira Kikapu Tanzania(TBF) imetangaza rasmi tarehe ya mashindano ya kikapu ya FIBA Zone V U18 (Wanawake na Wanaume ) kuwa yanatarajiwa kuanza June 17 hadi 22 2018 hapa Jijini Dar Es Salaam, Tanzania. 

Rais wa TBF Pharess Magesa amesema matarajio yao ni kuwa mmoja kati viongozi wetu wakuu wa nchi ndyie atakuwa mgeni rasmi wa mashindano hayo na yatarushwa mubashara (live) siku zote za mashindano na vituo vyote vikubwa vya TV na Radio ambavyo wametuma maombi.

Magesa amesema gharama za maandalizi ya timu zetu mbili za Taifa  na gharama za kuandaa mashindano haya ni kubwa, na tayari kuna wadau wameshajitokeza kutoa ahadi na wengine wameshasaidia. 

"Hadi sasa hivi TBF ina upungufu wa takribani Sh.milioni 100, kati ya hizo Sh.milioni 60 ni za kuandaa mashindano na Sh.milioni 40 ni za kuweka timu zetu 2 za wanawake na wanaume kambini na kununua vifaa vya michezo zikiwemo Jersey za kucheza na za mazoezi, truck suits, viatu, socks, mipira na madawa,"amesema Magesa. 

"Pia, tuna mahitaji mengi ili kufanikisha matengenezo ya uwanja wa ndani wa Taifa (indoor) ukiacha kuvuja paa na kukatika kwa umeme ambako kutadhibitiwa na msaada ulitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda,"amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...