Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Elias Kwandikwa, akizungumza na
wananchi wa mtaa wa Mpamaa, Kata ya Miyuji (hawapo pichani), kuhusu
mpango wa Serikali wa kulipa fidia kwa wananchi waliopisha ujenzi wa
Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, mkoani Dodoma. Kulia ni
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana na Ajira ambaye pia ni
Mbunge wa Dodoma mjini, Mhe. Anthony Mavunde.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana na Ajira ambaye pia ni
Mbunge wa Dodoma mjini, Mhe. Anthony Mavunde akifafanua jambo kwa
wananchi wa Kata ya Miyuji, Makutupora, Msalato na Nzuguni waliopisha
ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, mkoani Dodoma.
Wananchi wa Kata ya Miyuji, Makutupora, Msalato na Nzuguni
wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Elias Kwandikwa
(hayupo pichani), kuhusu mpango wa Serikali wa kulipa fidia kwa wananchi
waliopisha ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato,
mkoani Dodoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Elias Kwandikwa, akisalimiana na wazee wa
mtaa wa Mpamaa, Kata ya Miyuji mara baada ya kuzungumza nao kuhusu
mpango wa Serikali wa kulipa fidia kwa wananchi waliopisha ujenzi wa
Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, mkoani Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...