Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii 
Kanda ya Kaskazini.
SERIKALI imeziagiza Halmashauri kuhakikisha Maafisa Habari wanaingia katika vikao vya maamuzi ili waweze kupata na kutoa habari sahihi huku akiwatuhumu baadhi ya maafisa wa Halmashauri kuwa huendi ndio wanazuia maafisa habari kuingia katika vikao kwa lengo la kuficha baadhi ya taarifa.

 Agizo hilo la serikali limetolewa na Waziri wa nchi ofisi ya Rais ,Serikaliza Mitaa(TAMISEMI) Seleman Jafo wakati wa kufunga kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kilichofanyika jijini Arusha kwa muda wa siku tano.

 afo pia ameziagiza Halmashauri kutenga fungu katika Bajeti zao kwa ajili ya ununuzi wa vifaa kwa ajili ya Maafisa Habari ili kusaidia katika kutekeleza majukumu yao kwa urahisi ya kuhabarisha umma shughuli mbalimbali za maendeleo zinazofanywa Serikali. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akizungumza wakati wa kufunga Kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kilichofanika kwa siku tano katika Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa (AICC) jijini Arusha.
Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabodhi cheti kwa Mwenyekiti Mstaafu wa TAGCO ,Innocent Mungi ikiwa ni ishara ya utambuzi wa mchango wake katika chama hicho. 
Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabodhi cheti kwa Mmoja wa viongozi wa zamani wa TAGCO,Silvia Lupembe ambaye pia ni Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Chuo Kikuu cha Mzumbe ,Morogoroikiwa ni ishara ya utambuzi wa mchango wake katika chama hicho. 
Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabodhi cheti Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO) Leila Muhaji kutambua mchango wa Shirika hilo katika kufanikisha kikao kazi cha maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano  Serikalini kilichofanyika jijini Arusha. 

Mgeni rasmi katika ufugaji wa Kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini ,Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemeni Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...