Ecobank nchini Tanzania kuanzia mwaka huu inaanzisha mpango wa kutoa zawadi ya ufadhili kwa wasichana wanaofanya vyema katika masomo yao kwenye shule za serikali. Aidha pamoja na ufadhili huo ili kuwaweka katika hali ya kuwa na uzoefu na kazi zao wanazosomea, watakuwa wanahakikisha wakati wa likizo wanawafanyia mpango wa kujishughulisha na kazi hizo ili kuwa na uzoefu.

Hayo yamesema na Mkurugenzi Mkuu benki hiyo nchini Mwanahiba Mzee wakati wa hafla ya mchapalo iliyofanyika hoteli ya Serena kusherehekea mafanikio ya mwanamke katika Siku ya Wanawake duniani mwishoni mwa wiki. Alisema taasisi yake inaona umuhimu wa kumwezesha mtoto wa kike kusonga mbele kama moto wa taasisi hiyo ya kifedha unavyosema ‘press for progress’ ikimaananisha kujikita katika kutafuta maendeleo.
Mkurugenzi Mkuu Ecobank Tanzania, Mwanahiba Mzee akizungumza kabla ya mgeni rasmi ambapo alielezea kwa undani safari ya maisha kama mwanamke wakati hafla mchapalo ya kusherehekea mafanikio ya mwanamke katika Siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Ecobank Tanzania na kufanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Alisema mwanamke anafanyakazi nyingi hivyo ni vyema kumwandaa tangu mapema ili kujua majukumu yake kama mzalishaji mkuu kwenye familia.

Alisema kwa sasa hawajaamua wanaanzia ngazi gani za ufadhili, lakini wanataka kufanya kitu tofauti chenye kulenga kupromoti maendeleo ya mtoto wa kike kama maazimio ya Beijing yanavyotaka kufikia asilimia hamsini kwa hamsini katika ngazi za kiutendaji.

Alisema sherehe hiyo ambayo inaambatana na siku ya mwanamke duniani inasherehekewa katika nchi 33 zenye benki hiyo ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kibenki wa kuhakikisha kwamba wanawake wanasonga mbele kwa kuwa idadi yao ni asilimia 49.55 ya watu waliopo duniani na wanahaki ya kusaidia kukua kwa uchumi wa dunia, wa kaya na wakwao wenyewe kwa kuwezeshwa.
Mshehereshaji Babbie Kabae (kulia) akitambulisha wageni waalikwa kwenye hafla mchapalo ya kusherehekea mafanikio ya mwanamke katika Siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Ecobank Tanzania na kufanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Anasema pamoja na ukweli kuwa wanawake wameachwa nyuma kwa miaka mingi, taasisi hiyo imejipanga kuhakikisha kwamba inakuwa na asilimia 50 kwa 50 ifikapo mwaka 2030 huku hapa nchini inakaribia asilimia 49.

Alisema wakati sherehe hiyo ni kusherehekea mafanikio na kujifunza kutoka kwa wanawake waliofanya vyema, wanawake wanatakiwa kujiuliza wamesaidiaje wanawake wenzao kufikia ngazi ya juu kabisa ya uwezo walionao.

Alisema katika taasisi yake wametengeneza mpango wenye vipengele vitano vya kuhakikisha kwamba suala la jinsia linazingatiwa. Alitaja vipengele hivyo kama kushawishi fikira za jinsia katika maeneo ya kazi kuona kwamba kuna mizania. Kukabili fikira mgando dhidi ya wanawake, kuwezesha mwanamke kuonekana wazi, kushawishi kuinua wanawake kwa kutwaa huduma bora wanazozitoa na kusherehekea mafanikio ya mwanamke.
Mgeni rasmi Mwanasiasa Mkongwe nchini na mpigania haki za wanawake, Mama Getrude Mongella akitoa nasaha zake kwa wageni waalikwa na wafanyakazi wa Ecobank Tanzania (hawapo pichani) wakati wa hafla mchapalo ya kusherehekea mafanikio ya mwanamke katika Siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Ecobank Tanzania na kufanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Alisema amefurahishwa na jinsi wanawake majasiri kama Getrude Mongella walivyoweza kupigania haki za wanawake wakikabiliana na makandokando yake na kufanikisha maazimio ya Beijing ambayo yanatumika kumkomboa mwanamke.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...